JE ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA ?
Kuna
huu msemo wa siku nying unaosema "Elimu ni ufunguo wa maisha" Kama ni
kweli elimu mi ufunguo wa maiha basi kuna nyumba inaitwa MAISHA. Pamoja
kuwepo kwa nyumba hii nadhani wengi hatujaweza kufikia na kufungua ili
kupakua maisha yaliyoko humo ndani ya nyumba hii. pamoja na kuwa bado
kiwango cha wasomi nchini ni kidogo kulinganisha na wingi wa watu
tulionao basi hata hawa wachache tuliyomo bado hatujafikia nyumba
MAISHA. Unafikiri kwanini watu wamesoma na bado maisha yanawapiga
chenga? Najaribu kujiuliza baadhi ya maswali :Je tatizo ni mfumo wa
elimu yetu?Je tatizo ni wenye elimu? Au tatizo ni watoa elimu
(wakufunzi)? Kwa mtazamo wangu nadhani tatizo liko kwa waliosoma.
Mojawapo ya sifa kubwa ya mtu aliyesoma ni kuogopa kudhubutu
kupoteza.(Risk averses). Tatizo lingine la mtu aliyesoma ni kukukariri
kuwa ukimaliza shule lazima uajiriwe, pamoja na mtazamo huo kutokuwa
mbaya lakini lingine linalowakumba ni kuingia kwenye dhambi ya
kulalamika na kunungunikia serikali. watu tuliosoma tuna tabia ya
kulalamika sana badala ya kutafutanjia mbadala. Watu tuliosoma tumefaulu
vizuri vyeti vinapendeza sana lakini tumefeli kumudu maisha au kusaidia
watu wasio soma kuamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha. Ni kweli elimu
ni ufunguo wa maisha , mimi sina ubishi juu ya hili hata kidogo.
Tukisema elimu ni ufunguo wa maisha ni kweli kwa sababu zifuatazo:
Kabisa elimu (kwenda shule) ndikokuliko anza kukukutanisha na watoto
wenzako na kuanza kushirikiana tabia na kujifunza tofauti ya maisha ya
baba na mama yako, Pili baada ya kwenda sekonndari ndipo ukaanza
kukutana na watu wa makabila tofauti tofauti na ukajifunza zaidi ,Tatu
ulivyoenda chuo ukazidi kukutana na watu wazima kama wewe na kujifunza
zaidi tabia , miendendo na uweledi au utaalamu na katika kujifunza huko
ulikutana na simulizi mabali mabali kutoka kwa wakufunzi na wanachuo
wenzako. Mpaka hapo umepata ufunguo wa kukutana na watu mbalimbali na
kujua tamaduni mabali mabali na hulka za watu mabali. Huo ni ufunguo
mojawapo. Lakini n kubw zaidiumesoma vitabu mbali mbali za wataalamu
walio hai na wengine waliokufa na ukapata ujuzi waliotumia kumudu maisha
. Kufikia hapo nadhani huna ubisha kuwa elimu haijakuwa ufunguo wa
maisha. Sasa ufunguo mkubwa ni utaalam ulio pata shuleni au chuoni , je
huu unatumiaje kufungulia nyumba inayoitwa maisha? Nyumba maisha ina
tafsiri nyingi kwa msomi, inaweza kuwa mazingira yaliyokuzunguka ,
inaweza kuwa kituo chako cha kazi, inaweza kuwa siasa, inaweza pia kuwa
mwenendo wako kwa ujumla. Elimu ni ufunguo wa maisha hakuna ubishi, acha
kulalamikia serkali, acha kujilaumu, acha kungunika, acha kulalamikia
ukosefu wa mtaji. Tumia elimu kukabili a kutatua changamoto.

KAMA ELMU NI UFUNGUO UMEFUNGUA MLANGO UPI?
ReplyDeleteTumeona kuwa elimu ni ufunguo wa maisha kwani inaanza kukufungulia mlanago wa kukutana na watoto amabao sio Ndugu wala hakuna uko Nao na hatimaye kukutanisha na way mbali mbali kwenye upeo tofauti tofauti hadi kukutanisha na wataalamu watakaokupa utaalamu wa kukufanya uwe na ujuzi au utaalamu ambayo ndiyo hasa ufunguo wa kuweza kukufungulia Nyumba maisha.He Nyumba inayoitwa maisha ni IPI?Nyumba maisha ni mahali popote utakapokuwa ,ni mazingira yeyote utakayokuwa,uwe kazini uwe nyumbani au mahali popote hakikisha unatumia elimu yako kupambanua mazingira,hakikisha unatafuta changamoto zilizoko kwenye mazingira uliyoko na kwa kutambua changamoto tumia elimu au ujuzi uliyonao kugeuza changamoto kuwa fursa na chanzo cha kipato.Kwa kufanya hivyo utakuwa umefungua Nyumba inayoitwa maisha.Ukitaka kuonana ufunguo wako haufanyi Kazi anza kulalamikia mazingira uliyoko au anza kulaumu watu wanaokuzunguka au kulaumu viongozi au serikali! Hakikisha unafanya mambo kwa mtazamo chanya na sio hasi wala lawama.Ukiona unaanza kulaumu mazingira na watu au serikali Juma karibu utapoteza mwelekeo na ufunguo wako(elimu).Kama unaona elimu uliyonayo haendani na mazingira uliyoko na fursa unaziona basi tafuta elimu inayofuatana na mazingira uliyopo! Mfano kuna MTU mmoja alisomea mambo yabkuunga vyuma lakini akawa kijijini na mule hakuna vyuma wala karakana akakwa hajui pa kuanzia wala pa kutumia ujuzi alionao! Mwisho akaamu a kuchimba bwawa na kuvuna Maji ya mvua kwa msimu na pole pole aliyahifadhi hayo Maji na kuanzia kuyatumia wskati wakiangazi kuotesha mboga na niche michache ya migomba.Wskati wakiangazinkumekauka kabisa alianza kuwauzia watu mboga na kufunga wlndege na akaanza kutengenza kipato na mwisho alibadili fikra na mtazamo wa watu juu yake. Katika mazingira hayo alianza kujifunza Kilimo cha mboga mboga na kuweza kuwa utaalamu wa mboga na matunda na hatimaye akawa mshauri mkubwa wa lishe na Kilimo mboga mboga.Acha kulalamika kuwa mbunifu,!!
UFUNGUO WA MAISHA UMEFUNGULIA MLANGO UPI?
ReplyDeleteKama yulivyoona kuwa elimu ni ufunguo wa maisha na unaweza kuwa una elimu lakini huoni mlango wa kufungulia.Sababu kubwa ni kwamba pengine ulichukua ufunguo ambayo hujui kutumia au mpaka uone MLANGO wa kufungulia kunahitaji tufanye Kazi ya ziada! Kuna watu wamesoma elimu wasioipenda au wasiojua wapi pa kutumia ,wamesoma tu kwa msukumo wa wazazi au marafiki lakini pengine hawapendi au walijikuta tu wamepangiwa kusoma na serikali! Ukitaka ufunguo wako ufungue kila MLANGO basi Fanya au soma kitu kinachotoka moyoni kwako na sio vinginevyo.Kwa kufanya hivyo utakuwa umefungulia elimu yako MLANGO uliosahihi!Ukitaka kufanikiwa katika maisha Fanya mambo yafuatayo: Kwanza hakikisha una Imani sahihi juu ya Mungu unaye kwanini,pili hakikisha unakaa Katibu na watu waliofanikiwa kwa kutumia elimu yao inayofanana na yako,tatu wadadasi mbinu au kanuni walizofuata kufanikuwa,tatu hakikisha hujidharau mwenyewe,nne usikubali mazingira yakutawale,tano hakikisha neno sitaweza haliko akilini kwako,sita kaa mbali na walioshindwa na wakatisha tamaa,saba sikiliza nafasi yako katika kutenda Yale unayofikiri, Nane usiache kujifunza kwa tusafiri au kusoma Vitabu,Tisa jifunze kutoka baada ya kufanikiwa,kumi mafanikio yasikutenge na watu wala Mungu. Hayo ni baadhi tu ya mambo ambayo yanweza kukufanya ufunguo wako wa maisha tufanye Kazi vizuri! Kwa kufuata hizo kanuni ufunguo wako wa maisha utafungua kila MLANGO wa mafanikio.Pia jifunze kutokuwa mbinafsi.Nakutakia mafanikio mema na uwe na wskati mwema wa kujifunza
KAMA ELIMU NI UFUNGUO KWANINI WATU WENGINEWATUMIE UFUNGUO WAKO?
DeleteWatu wengine tuliosoma hatupendi kutumia elimu kwa manufaa yetu isipokuwa tunakimbilia kutimiza ndiyo na maono ya watu wengine! Kwa lugha nyingine tunatumia elimu yetu kuwafungulia wengine milango yako ya naisha.Fikiri unasoma unawaza tu kutumia na watu wabunifu tena wasio na utaalamu ulio Nao!Sikiliza ajira ni njia sahihi ya kusikia umasikini wa kipato! Na ajira ni ajira tu hata ubadilishe mwajiri ni sawa na kubadili njia ya unayotumia kusafiria kuelekea katika umasikini wa kipato!Sina maana ya kuchukua ajira ila tunapoajiriwa tuache kuwaza mshahara kuongezeka tu,fikiria jinsi ya kuongea kipato na njia halali za kupata kipato! "Employment is never certain" Ukitengeneza milango yako ya hela umetengeneza kofuli LA Nyumba yako ambayo ufunguo unajua kutengeza mwenyewe pia hivyo hutakaa ushindwe kufunga! Amka acha kufungulia watu maisha fungua ya kwako mwenyewe! Tuma elimu kwa manufaa yako na wengine!